Mahabusu afariki muda mfupi baada ya kupewa dhamana mkoani Tabora.




Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Ndatulu Sangaya miaka 33 mkazi wa kijiji cha Ipembe wilayani Igunga Tabora amefariki dunia katika mahabusu ya mahakama ya mwanzo ya Mwamashere wilayani Kishapu
Shinyanga muda mfupi baada ya kupata mdhamana kwa tuhuma za kumshambulia mtu mmoja na kumdhuru mwili wake.
Akithibitisha kifo cha mtu huyo kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Mika Nyange ameeleza kuwa mnamo tarehe kumi na tano mwezi wa kwanza mwaka huu mtuhumiwa akiwa na baba yake mzazi aitwaye Sagaya Shishi walimshambulia mtu mmoja mkazi wa kijiji cha Ipembe wilayani Igunga na hatimaye kukimbilia wilayani Kishapu mkoani Shinyanga ambapo walikamatwa na kufikishwa katika mahakama ya mwanzo ya Ukenyenge na muda mfupi baada ya kupewa dhamana hali yake ilibadilika ghafla na kufariki dunia.
Aidha kamanda Nyange ameeleza kuwa hali ya mtuhumiwa ilipoonekana kuwa mbaya alikimbizwa katika zahanati ya Mwamashele tarafa ya Ukenyenge Kishapu na kupatiwa matibabu lakini afya yake ilizidi kuwa mbaya hali iliyosababisha kifo chake na jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi kuhusiana na kifo hicho.

source:ITV

0/Post a Comment/Comments

Stay Conneted

{ads}