
Tunapenda
kutoa taarifa kwa Umma kuwa, Barabara ya Mpanda – Koga – Tabora
imefungwa kwa muda kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini
zilizosababisha kufurika kwa mto Koga na kufanya daraja la Koga,
lililopo mpakani mwa Mikoa ya Katavi na Tabora kutopitika na hivyo
kukata mawasiliano ya barabara katika mikoa hiyo
Kutokana
na kukatika kwa mawasiliano ya barabara kupitia daraja hilo, tunaomba
wananchi kusitisha safari kwa kutumia barabara hiyo ili kuepusha madhara
yanayoweza kujitokeza hadi hapo barabara hiyo itakapofunguliwa mara tu
baada ya maji kupungua katika eneo hilo.
Wizara
ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imechukua hatua hiyo kwa mujibu wa
Kifungu cha 41 (1) cha Sheria ya Barabara Na. 13 ya Mwaka 2007 na Kanuni
ya 8 (1) ya Kanuni za Usimamizi za Barabara za Mwaka 2009.
Wizara, inaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza katika kipindi hiki chote.
Imetolewa na:
Eng. Joseph Nyamhanga
KATIBU MKUU (UJENZI)
28/01/2016

Post a Comment